Habari Mpya :

Habari Mpya

MATUKIO YA PICHA KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO

Imeandikwa na Henry Mdimu on Saturday, May 25, 2013 | 19:20

Mbunge wa Nyamagana Mhe. Ezekia Wenje (CHADEMA), akichangia mjadala wa Hotuba ya  Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 Bungeni leo. 2 
Mbunge wa Geita Mhe. William Ngeleja (CCM) , akichangia mjadala wa Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 Bungeni leo. 3 
Wabunge wa Viti Maalumu CHADEMA, Mhe. Joyce Nkya(aliyekaa) na Mhe. Lucy Owenya (aliyesimama) wakizungumza jambo wakati wa kikao cha Bunge wakati wa mjadala wa Hotua ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2013/2014. 4   
Mbunge wa Msalala Mhe. Ezekiel  Maige (CCM),  akichangia mjadala wa Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 Bungeni leo. 5 
Mbunge wa Muleba Kaskazini  Mhe. Charles Mujage (CCM),  akichangia mjadala wa Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa Fedha 2013/2014 Bungeni leo. 6 
Mbunge wa Longido mhe. Michael Laizer (CCM), akisikiliza kwa makini hoja zinazotolewa katika uchangiaji wa mjadala wa Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. 7 
Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo (kushoto) akiwa na Manaibu wake  mhe. Stephen Masele(katikati)  na Mhe. George Simbachawene wakisikiliza hoja za wabunge katika mjadala wa Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini leo Bungeni. Juu ni Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makaazi Mhe prof. Anna  Tibaijuka.

JAMANI JAMANI WAENDESHA BODABODA KUWENI MAKINI WENZENU HAWAWAJALI

Taarifa hii ni kwa hisani ya blog ya FULL SHANGWE

Lori aina ya Fuso likiwa limemgongandesha pikipiki aliyekuwa inakatiza kwenye taa nyekundu leo kwenye njia panda ya Segerea. 3 
Dereva wa pikipiki  hiyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja akiuguli maumivu kabla ya kupatiwa msaada wa kukimbizwa hospitali.
4 

VIONGOZI WA CCM VYUONI WAKUTANA OFISI NDOGO LUMUMBA LEO

Kaimu Mwenyekiti vyuo vikuu, wilaya ya Dar es salaam, Assenga Abubakar (Kushoto),Katibu Msaidizi Mkoa wa vyuo vikuu,anayeshughulikia  na mikoa ya Dar es salaam na Zanzibar na Kepteni mstaafu,Alhaji Mohamed Ligola wakiwa kwenye mkutano na viongozi wa matawi ya vyuo ya CCM DSM.
7 
Baadhi ya viongozi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu mkoa wa Dar es salaam wakiwa kwenye mkutano wao ambao pamoja na kujadili masuala mbali mbali ya kisiasa na masaula ya gesi Mtwara pia walipata wasaa wa kupata Darasa la Itikadi.

TAARIFA ZA KMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU (TFF)


tff_LOGO1 
30 TWIGA STARS WAITWA KAMBINI
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twiga Stars), Rogasian Kaijage amewaita kambini wachezaji 30 ikiwa ni mwendelezo wa kuijenga na kuiimarisha timu hiyo.

Twiga Stars itakuwa na kambi ya siku kumi kuanzia Jumapili (Mei 26 mwaka huu) ambapo baadaye inatarajia kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya wachezaji kurudi kwenye klabu zao.

Kambi hiyo ni mwendelezo wa programu iliyopendekezwa na kocha kuijenga na kuiimarisha timu hiyo kwa vile haina mashindano mwaka huu, na itakuwa kambi ya pili baada ya ile iliyofanyika Machi mwaka huu.

Wachezaji walioitwa na klabu zao kwenye mabano ni Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar), Belina Julius (Lord Barden), Ester Chabruma (Sayari), Ester Mayala (TSC Academy), Eto Mlenzi (JKT), Evelyn Sekikubo (Mburahati Queens) na Fatuma Bushiri (Mburahati Queens).

Fatuma Hassan (Mburahati Queens), Fatuma Omari (Sayari), Flora Kayanda (Tanzanite), Hamisa Athuman (Marsh Academy), Hellen Peter (JKT), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Tanzanite), Mwanahamisi Omari (Mburahati Queens), Mwanaidi Tamba (Mburahati Queens) na Mwapewa Mtumwa (Sayari).

Nabila Ahmed (Marsh Academy), Pulkeria Charaji (Sayari), Rehema Abdul (Lord Barden), Rukia Khamis (Uzuri Queens), Semeni Abeid (Tanzanite), Sharida Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Sayari), Therese Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).

RCL KUENDELEA KUTIMUA VUMBI KESHO
Raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaendelea kesho (Mei 26 mwaka huu) kwa mechi sita za kwanza zitakazochezwa katika miji sita tofauti.


Abajalo ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam wakati Machava FC ya Kilimanjaro itakuwa mwenyeji wa Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.

Nayo Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida huku Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara ikimenyana na Biharamulo FC ya Kagera kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.

Mjini Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi Warriors ya Katavi wakati Njombe Mji itaikaribisha Kimondo SC ya Mbeya kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

Leo (Mei 25 mwaka huu) Friends Rangers ya Kinondoni, Dar es Salaam inacheza na African Sports ya Tanga kwenye Uwanja wa Azam Chamazi. Mechi za marudiano zitachezwa kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na 9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

RAIS KIKWETE KATIKA MKUTANO WA SHEREHE ZA MIAKA 50 YA AU JIJINI ADDIS ABABA LEO

Muono wa jicho la samaki katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013PICHA NA IKULU au7 
Marais Wastaafu wakiwa katika Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013 au11 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mkutano wa Sherehe za miaka 50 ya AU katika makao makuu ya umoja huo jijini Addis Ababa leo Mei 25, 2013

Sudan Kusini haitashirikiana na mahakama ya ICC

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametoa mwito kwa bara la Afrika kusimama kidete na kwa umoja, kujiamulia maswala yake yenyewe.
 Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir  na rais wa Kenya  Uhuru Kenyatta, mjini Juba, Mei 23, 2013.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, mjini Juba, Mei 23, 2013.

Rais wa Sudan Salva Kiir amesema Alhamis kuwa kamwe hatakubali kuingia katika mkataba wa mahakama ya uhalifu wa kivita-ICC. Bw. Kiir alikuwa akizungumza baada ya kutembelewa na rais mpya wa Kenya, bw. Uhuru Kenyatta aliyeahidi kuunga mkono ujenzi wa barabara, njia za reli na mabomba ya mafuta, ili kuboresha mahusiano ya kiuchumi kati ya Kenya na taifa hilo jipya.
Hii ilikuwa ziara ya kwanza kwa rais Uhuru Kenyatta huko Sudan Kusini tangu alipoapishwa kuwa rais wa Kenya na alikaribishwa kama ndugu na rais Kiir aliyemweleza ajihisi kuwa nyumbani.

Rais Kiir aliahidi kusimama wima na kiongozi wa Kenya na wananchi wa Kenya. Bw. Kenyatta alichukua madaraka baada ya kushinda uchaguzi wa kiti cha urais mwezi Machi, wakati huo akiwa bado anakabiliwa na kesi katika mahakama ya ICC, inayomshtumu kwamba alichochea ghasia za uchaguzi  wa mwaka wa 2007.

Lakini huku mataifa ya Magharibi yakisita kumpongeza kufuatia ushindi wake, viongozi wengi wa Afrika walimpongeza na kuahidi kumuunga mkono kwa hali na mali bila kujali mashtaka ya mahakama ya The Hague.

Alhamis rais Kiir aliipuzilia mbali mahakama hiyo ya ICC na kusema Sudan Kusini haina nia ya kutia saini mkataba wa  kushirikiana nayo na hivyo kuchukua msimamo sawa na wa viongozi wengine wengi wa bara la  Afrika wanaosema mahakama hiyo inalenga waafrika. Alisema jamii ya kimataifa imekuwa ikiirai nchi yake kutia saini mkataba na ICC ili ipewe msaada lakini wamesema kamwe hawakubali.

Bw. Kiir alisema viongozi wa Afrika watajadilia  zaidi swala la Kenya na ICC katika mkutano wa mwishoni mwa wiki wakati wa kongamano kuu la Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa, Ethiopia wakati wa maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo la Umoja wa Afrika. Alisema viongozi wa Afrika watanena kwa sauti moja na kusimama wima na ndugu na dada zao wa Kenya.

Katika hotuba yake rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta alitoa mwito kwa bara la Afrika kusimama kidete na kwa umoja, kujiamulia maswala yake yenyewe.

Idadi ya wakimbizi yaongezeka duniani

Amnesty International yataja DRC, Ivory Coast, Sudan na Sudan Kusini kuwa miongoni mwa nchi zinazokiuka haki za binadamu.
Wakimbizi wa Sudan Kusini
Wakimbizi wa Sudan Kusini

Ripoti ya kila mwaka ya shirika la kutetea haki za binadamu, Amnesty International, inaelezea jinsi idadi ya wakimbizi  imeongezeka  kote duniani na jinsi  jamii ya kimataifa imeshindwa kuwasaidia, hili likiwa mojawapo ya swala kuu la haki za binadamu  kwa muda wa mwaka mmoja uliopita.
Shirika hili lenye makao ya London, limeelezea mtandao wa internet kama kifaa muhimu cha kupigana dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu. Amnesty International inasema idadi ya wakimbizi iliongezeka na kufikia milioni 15 mwaka jana huku mamilioni ya wengine wakitoroshwa manyumbani mwao na kuhamia sehemu nyingine za nchi  zao ambapo wanaishi kwenye kambi.

Hali hiyo yaripotiwa kuzorota zaidi barani Afrika hususan katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Ivory Coast, Sudan na Sudan Kusini. Lakini kando na nchi zinazokiuka haki za binadamu na kusababisha raia kukimbia, Amnesty International pia linashtumu nchi zinazopokea wakimbizi hao kwa kushindwa kuwasadia inavyopaswa.

Salil Shetty, katibu mkuu wa shirika hilo aliiambia Sauti ya Amerika kuwa  serikali husika zinazopokea wakimbizi hutoa kipaumbele katika kulinda mipaka yake na maslahi yake ya kitaifa  kuliko kulinda haki za  binadamu.

Shirika hilo pia lilitoa hati zinazoonyesha mateso na ukandamizaji katika zaidi ya nchi 100 huku 57 zikiwa na wafungwa wa kisiasa. Shetty anasema matumizi ya teknolojia ya mawasiliano kama vile simu za mkononi, kamera za video na mitandao ya kijamii kama  Twitter, imesaidia kuonyesha ukatili unaofanywa dhidi ya binadamu.

Alitoa mfano wa kamera za simu za mkononi ambazo zimetumiwa kurekodi mashambulizi ya raia nchini Syria pamoja na ukiukwaji wa haki za binadamu. Amnesty International inasema  japo ripoti na kanda hizo hazizuii  mashambulizi hayo, zinaonyesha dunia kile ambacho kisingewezekana miaka ya nyuma na huenda zikazuia manyanyaso na ukiukwaji katika siku zijazo .

Matumaini ya Afrika katika miaka 50 ijayo

Mataifa ya Afrika yanasherehekea miaka 50 tangu kuundwa kwa umoja wa nchi huru za Afrika , OAU, leo (25.05.2013)jumuiya iliyokusudiwa kuleta umoja wa bara hilo. 

Mfalme Haille selassie wa Ethiopia na wakuu wa nchi na serikali 31 walikutana mjini Addis Ababa tarehe 25, mwezi wa Mei kuizindua jumuiya hiyo mwaka 1963. Uzinduzi wa OAU , Umoja wa nchi huru za Afrika miaka 50 iliyopita unaadhimisha hatua muhimu ya kihistoria kwa bara zima, ambalo lilikuwa wakati huo likipitia kwa haraka katika kipindi cha kutoka katika ukoloni.

Mfalme Haille Selassie na viongozi wengine wa mataifa ya Afrika na serikali waliasisi umoja huo mjini Addis Ababa.

Eine Ehrenformation steht zum Empfang der ankommenden Konferenzteilnehmer auf dem Flughafen von Addis Abba. Am 25. Mai 1963 wurde in der äthiopischen Hauptstadt Addis Abeba die Organisation Afrikanischer Einheit (OAU) gegründet.
Gwaride la kuwakaribisha viongozi wa Afrika mjini Addis Ababa mwaka 1963
 
Makucha ya ukoloni
Wengi wa viongozi ambao walikuwapo wakati huo wameweza hivi karibuni tu kujitenga na hisia za kikoloni na wanatafuta njia kwa nchi zao kujenga upya mifumo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi iliyoporomoka kwa kutaka kushirikiana zaidi na majirani zao.

Upande wa kusini , makoloni ya Ureno ya Angola na Msumbuji bado yanakabiliwa na hali ya kujitoa kutoka katika zaidi ya muongo mmoja wa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

Hatua hiyo ni ndefu zaidi kwa hali ya baadaye ya Zimbabwe na Namibia, ambapo nchi hiyo ilikuwa inadhibitiwa na Afrika kusini ya kibaguzi wakati huo, na ilichukua zaidi ya miaka 30 kabla ya Afrika kusini binafsi kufikia serikali ya kidemokrasia.

Maadhimisho
Mkusanyiko huu wa kihistoria leo(25.05.2013) ni ishara ya ndoto za bara ambalo limenyonywa vya kutosha.
Kwa Waafrika wengi ndoto hizo bado hazijatimia licha ya matumaini ya muda huo na juhudi kubwa tangu wakati huo.

Der äthiopische Kaiser in einer undatierten Aufnahme. Kaiser Haile Selassie wurde am 23. Juli 1892 in Edjersso als Prinz Tafari Makonnen geboren. Am 2. November 1930 ließ er sich zum Kaiser krönen. Nach dem erfolgreichen Abessinien-Feldzug der Italiener floh er 1936 ins britische Exil, kehrte jedoch 1941 mit britischen Truppen zurück und zog am 5. Mai 1941 wieder in Addis Abeba ein. Innenpolitisch nicht sehr erfolgreich, verfolgte er eine rege Reisediplomatie. Die Gründung der Organisation für afrikanische Einheit (OAU) im Mai 1963 in Addis Abeba war hauptsächlich sein Werk. Anfang Juli 1974 übernahmen die Miltärs die Macht und setzten ihn am 12. September 1974 formell als Kaiser ab. Die folgenden Jahre verbrachte Haile Selassie unter strengem Hausarrest im Menelik-Palast in Addis Abeba, wo er am 27. August 1975 starb, wobei sich stets die Vermutung hielt, das er einem Mordanschlag zum Opfer gefallen war. Marehemu mfalme Haile Selassie wa Ethiopia

Katika hotuba yake kwa viongozi waasisi wa OAU, Haille Selassie alikumbusha udhalilishaji uliofanyika hapo kabla. 

"Kipindi cha ukoloni ambacho tulitumbukizwa , kilitufikisha mahali bara hili kudhibitiwa na wakoloni , na watu wetu ambao walikuwa huru na wenye kujisikia fahari kudhalilishwa na kuwa watumwa." amesema.

"Leo Afrika imejitokeza kutoka katika njia hii ya giza. Mapambano yetu dhidi ya uovu yamekwisha.

Hali hii ilikuwapo katika baadhi ya sehemu za Afrika, ikiwa ni pamoja na Ethiopia yenyewe.Mfalme alitangaza kuwa bara hilo liko njiani kati ya Afrika ya kale na Afrika ya hapo baadaye. Wengi wangesema kuwa hali hiyo bado imeendelea hata baada ya miaka 50.

epa03084113 A handout image made available by the South African Government Communication and Information System (GCIS) shows a general view of the the new African Union building where the present 26th meeting of the NEPAD Heads of State and Government Orientation Committee (HSGOC) is being held, Addis Ababa, Ethiopia, 29 January 2012. EPA/Jacoline Prinsloo / GCIS / HANDOUT HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES Viongozi wa sasa wa Umoja wa Afrika mjini Addis Ababa

Waafrika wengi bado wana uhaba wa chakula na wanaishi katika umasikini uliokithiri. Mabadiliko ya hali ya hewa yameleta ukame na mafuriko. Ukosefu wa ajira ni mkubwa, huku kukiwa na matumaini machache kwa vijana katika maeneo mengi ya bara hilo.

Vita na mizozo
Mapigano yanaendelea nchini Mali, jamhuri ya kidemokrasi ya Congo na Sudan.

Libyan leader Moammar Gaddafi attends the opening of the African heads of State summit in Addis Ababa, Ethiopia on 02 February 2009. African heads of states and governments designated the Libyan leader Moammar Gaddafi to chair the African Union for one year. Gadhafi's election at the head of the African Union could give Libya the opportunity to follow closely the ongoing efforts to organize peace talks between Sudan government and Darfur main rebel movements EPA/SABRI ALMHEDWI +++(c) dpa - Report+++ Marehemu Muammar Gaddafi

Wanadiplomasia wa Afrika wanasema mradi wa kuiunganisha Afrika kuwa bara lenye amani si jambo lililoshindwa lakini ni hatua inayoendelea.

Umoja wa Afrika, AU ulianzishwa mjini Durban mwaka 2002 kuchukua nafasi ya Umoja wa nchi Huru za Afrika, OAU, kwa msukumo wa kiongozi wa zamani wa Libya Moammar Gaddafi.

United Nations troops patrol on the road to Sake, 27kms from the provincial capital of Goma, in the Democratic Republic of the Congo, on 04 November 2008. The United Nations and international aid organization are fighting an uphill battle to get help to over 250,000 people that are thought to have been forced from their homes and villages. EPA/STEPHEN MORRISON +++(c) dpa - Report+++
 
Wapiganaji wa M23 katika jamhuri ya kidemokrasi ya Congo

HABARI ZA BURUDANI

habari nyinginezo »

HABARI ZA KITAIFA

Habari nyinginezo »

HABARI ZA MICHEZO

habari nyinginezo »

HABARI ZA KIMATAIFA

habari nyinginezo »

HABARI ZA BIASHARA

Habari nyinginezo »
 
BLOG DESIGNERS : Bongoclan Blog Besigners | Anga Designers | Call us 0752184797
Copyright © 2011. Mdimu's Blog - All Rights Reserved
Template Modify by Eddie Sucre
Proudly powered by Blogger